Monday, April 25, 2011

Ban Kimoon Amtumia Salam Za Pongezi JK Za Miaka 47 Ya Muungano

MIAKA 47 YA MUUNGANO BAK KI MOON AMTUMIA SALAMU ZA PONGEZI RAIS

JAKAYA KIKWETE NA WATANZANIA-

NA MWANDISHI MAALUM

NEW YORK

Wakati watanzania wakiadhimisha hapo kesho miaka 47 ya Muungano.Katibu Mkuu

wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, Serikali na watanzania wote.

Katika salamu zake ambazo nakala yake ilitumwa katika Ubalozi wa Tanzania Umoja

wa Mataifa, Ban Ki Moon anasema , wakati huu kuliko ilivyokuwa wakati mwingine

wowote, dunia inakabiliwa na changamoto nyingi.

Amesema changamoto hizo ambazo zimevaa sura tofauti na uzito tofauti, zinavuka

mipaka kutoka taifa moja hadi lingine. Na kwamba kuzitafutia ufumbuzi kunataka

utulivu, umakini, mshikamano na ushirikiano wa kimataifa .

Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa, amemwelezea Rais Jakaya Kikwete kwamba,

yeye binafsi amedhamiria katika kuhakikisha kuwa Umoja wa Mataifa, unakwenda

sambamba na kasi ya mabadiliko yanayotokea hivi sasa duniani. Na kuhakikisha

kwamba Umoja wa Mataifa unasimamia na kutoa matarajio yenye kuridhisha na halisi

katika kazi zake tatu kuu za msingi ambazo ni maendeleo, amani na usalama na haki

za binadamu.

Ameeleza kuwa anafarijika na kutiwa moyo sana na uongozi unaojituma wa

ya Muungano wa Tanzania . Na kwamba anaihesabu Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania kama mshirika mkubwa katika kuifanya dunia kuwa endelevu na salama

kwa watu wote.

No comments:

Post a Comment